95 – Zileteni Zaka Kwa Hazina

( Bring Ye All The Tithes )

1. Sikieni neno la Mungu Wetu, Zileteni zaka kwa hazina
Leteni na mioyo yenu yote; mibaraka itakuja.

Zileteni zaka kwa hazina, kanijaribu sasa nazo;
Nitakupeni mibaraka, zaidi ya nafsi ya kupewa.

2. Wataka Roho Mtakatifu kwako? Uzilete zaka kwa hazina
Ukae karibu na Bwana wako, ndipo utakapo barikiwa.

3. Je! Unakasoro na Bwana wako? Uzilete zaka kwa hazina
Uzilete kama alivyosema, Ndipo utakapo barikiwa.

4. Ushukuru Bwana na moyo wote, unapoleta zaka ghalani;
Usadiki ahadi zake zote, ndipo utakapo barikiwa.

5. Tuimbe sote nyimbo za furaha, tunapoleta zaka ghalani
Twimbe kabisa na furaha kubwa, kwani tutabarikiwa.

WhatsApp