93 – Jua La Rohoni Mwangu

( 502 – Sun of My Soul )

1. Jua la rohoni mwangu, mpendwa Mwokozi wangu;
Usiku giza hapana, ukiwa karibu Bwana.

2. Nikipata usingizi, nijaze fikara hizi,
Ni tamu sana, nilale pendoni mwako milele.

3. Kaa nami, ewe Bwana, Usiku kama mchana,
Nisiishi mbali nawe; ni uhai kuwa nawe.

4. Kama mtoto mnyonge ameshawisha atange,
Mtafute Ewe Bwana, ujirudishie tena.

5. Wagonjwa wape amani, waneemeshe maskini,
Walio, Mtulizi, wape wote usingizi.

6. Asubuhi tutokapo, tukaribishe tulipo;
Twingiapo duniani tuwe mwako mkononi.

WhatsApp