91 – Kaa Nami

( 050 – Abide With Me )

1. Kaa nami, ni isiku tena;
Isiniache gizani, Bwana.
Msaada wako haukomi;
Nili peke yangu, kaa nami.

2. Siku zetu hazakawi kwisha;
Sioni la kunifurahisha;
Hakuna ambacho kakikomi,
Isiye na mwisho kaa nami.

3. Nina haja nawe kila saa;
Sina mwingine wa kunifaa
Mimi nitaongozwa na nani
Ila wewe? Bwana, kaa nami.

4. Sichi neno uwapo karibu;
Nipatalo lote si taabu;
Kifo na kaburi haviumi;
Nitashinda kwako, kaa nami.

5. Nilalapo nikuone wewe,
Gizani mote nimulikiwe;
Nuru za mbinguni hazikomi,
Siku zangu zote; kaa nami.

 

WhatsApp