75 – Msingi Imara, Ninyi Wa Bwana

( 509 – How Firm a Foundation )

1. Msingi imara, ninyi wa Bwana,
Ume wekwa kwenu kwa neno lake?
Nini zaidi atasema Bwana?
Imani yenu ipate kuzidi?

2. Wanbiwapo vuka maji ya giza,
Mito ya mashaka haitazidi;
‘Takuwapo nawe, nikuwezeshe,
Shida upatazo zisikutishe!

3. Utakapopishwa Ndani ya moto
Nguvu nitakupa, upate pato;
Huteketezwi, ila taka zako.
Na zitasalia dhahabu zako.

4. Na mtu aliyenitegemea
Nguvu za jehanamu zijapotisha,
Kamwe kwa adui sitamtia;
Mtu wangu kamwe sitamuacha.

WhatsApp