( Asked Not To Be Excused )
- Usikatae Kazi yake Bwana; Ukae tayari Kuifanya kazi;
Uende po pote Mungu akwitapo, Nawe utaona Furaha kazini.
Njoo, We! Usiikatae; Njoo, We! Uifanye kazi;
Usiikatae Kazi yake Bwana, Ili hatimaye usikatazwe juu.
- Usiikatae Kazi yake Bwana; Kwa nini kawia? Fanya kazi leo.
Mavuno meupe, Wachache Wavuni, Onyesha furaha Kwa kazi ya Bwana.
- Usiikatae Kazi yake Bwana, Kukataa pendo Kwako ni Hatari.
Saa ya rehema, Yesu akiomba, Ziungame dhambi, Zifutwe mbinguni.