(
369 – Bringing in the Sheaves )
- Twapanda mapema, na mchana kutwa
Mbegu za fadhili hata jioni,
Twangojea sasa siku za kuvuna;
Tutashangilia wenye mavuno.
Wenye mavuno, wenye mavuno,
Tutashangilia wenye mavuno.
Wenye mavuno, wenye mavuno,
Tutashangilia wenye mavuno.
- Twapanda mwangani na kwenye kivuli;
Tushindwe na baridi na pepo;
Punde itakwisha kazi yetu hapa:
Tutashangilia wenye mavuno.
- Twapanda kwa Bwana mbegu kila siku.
Tujapoona taabu na huzuni;
Tuishapo shinda atatupokea:
Tutashangilia wenye mavuno.