45 – Mwanga Umo Mwoyoni.

( Sunlight In The Heart )

1. Mlimani pana mwanga, Mwanga wa jua zuri
Shambani na baharini Jua tukufu liko;
Mwanga ulio mkubwa Umo moyoni mwangu,
Kwa kuwa Yesu alipo Hapa pana mwangaza.

Mwangaza ulio mzuri, Mwanga umo moyoni;
Akiwapo Bwana Yesu Pana mwanga moyoni.

2. Kama mavazi kukuu Ninavua huzuni:
Nguo nzuri za furaha Umenipa za kuvaa.
Nakuandama rohoni Hata nyuba ya juu
Iliyopambwa vizuri Katika pendo lako.

3. Ulinikomboa Yesu; Maisha yangu, mali,
Vyote ni nyako, Mwokozi—Daima nikusifu.
Nakuandama rohoni Hata nyumba ya juu
Iliyopambwa vizuri Katika pendo lako.

WhatsApp