29 – Yesu, Nakupenda

( 321 – My Jesus, I Love Thee )

1.Yesu nakupenda, U mali yangu,
Anasa za dhambi sitaki kwangu;
Na mwokozi aliyeniokoa
Sasa nakupenda, kuzidi pia.

2.Moyo umejaa mapenzi tele
Kwa vile ulivyonipenda mbele,
Uhai wako ukanitolea
Sasa nakupenda, kuzidi pia.

3.Ulipoangikwa Msalabani
Tusamehewe tulio ndambini;
Taji ya miiba uliyoivaa,
Sasa nakupenda, kuzidi pia.

4.Mawanda mazuri na masikani
Niyatazamapo huko mbinguni,
‘Tusema na taji nitakayovaa
Sasa nakupenda, kuzidi pia.

WhatsApp