24 – Jina La Yesu Tamu

( 238 – How Sweet the Name! )

1. Jina lake Yesu tamu Tukilisikia,
Hutupoza, tena hamu Hutuondolea.

2. Roho ilioumia Kwalo hutibika,
Chakula, njaani pia; Raha, tukichoka.

3. Jina hili ni msingi, Ngao, ngome, mwamba,
Kwa hili napata ungi, Kwangu ni akiba.

4. Yesu, Mchunga, Rafiki, Mwalimu, Kuhani,
Mwanzo, mwisho, na amina, mali yangu yote!

WhatsApp