176 – Ati Tuonane Mtoni?

( 432 – Shall We Gather at the River )

1. Ati twonane mtoni? maji mazuri ya mbingu;
Yanatokea mwangani, penye kiti cha Mungu.

Naam, twonane mtoni! Watakatifu, kwenu ni mtoni!
Tutakutanika kule mtoni penye kiti cha Mungu.

2. Tukitembea mtoni na Yesu mchunga wetu,
Daima tu ibadani usoni pake kwetu.

3. Tukisafiri mtoni tutue ulemeao,
Wema wa Mungu yakini: una taji na vao!

4. Kwang’ara sana mtoni cha Mwokozi ni kioo,
Milele hatuachani tumsifu kwa nyimbo.

5. Karibu sana mtoni, karibu tuatawasili,
Mara huwa furahani na amani ya kweli.

WhatsApp