175 – Uso Kwa Uso

( 206 – Face to Face )

1. Nitaonana na Yesu, uso kwa uso kweli;
Siku ile shangwe tele nitamwona Mwokozi.

Tutaonana kwa macho, huko kwetu mbinguni;
Na kwa utukufu wake, nitamwona milele.

2. Sasa siwezi kujua jinso alivyo hasa,
Bali atakapokuja, nitamwona halisi.

3. Mbele yake yafukuzwa machozi na huzuni;
Kipotovu kitanyoshwa, fumbo litafumbuka.

4. Uso kwa uso! Hakika palepale furaha;
Nitafurahi kabisa nikimwona Mwokozi.

WhatsApp