158 – U Mwendo Gani Nyumbani?

( 439 – How Far From Home )

1. U mwendo gani nyumbani? Mlinzi akanijibu,
“Usiku sasa waisha,mahe kaibu.”
Usihuzunike tena, bali ulemee mwendo
Hata ushike ufalme kule mwangani juu.

2. Na tena niliuliza, nchi yote ikajibu:
“Sasa mwendo watimika, milele karibu.”
Usihuzunike tena, ishara kuu zasonga
Na viumbe vyangojea sauti ya Bwana.

3. Nikamwuliza shujaa, ndivyo kanitia moyo:
“Shikilia mapigano, kitambo yaisha.”
Usihuzunike tena, kazi ifanye kwa moyo;
Tumeahidiwa tunu tuishapo shinda.

4. Siyo mbali na nyumbani! Fikara tamu njiani,
Latupoza roho, nalo lafuta machozi
Usihuzunike tena, kitambo tutakutana
Wenye furaha kamili nyumbani mwa Baba.

WhatsApp