154 – Yanipasa Kuwa Naye

( I Must Have The Saviour With Me )

1. Yanipasa kuwa naye, Mwokozi Bwana wangu,
Akiwa karibu nami, napata nguvu kweli.

Moyo hauogopi, wala kitikisika.
Nitakwenda apendapo. Kwa kuwa anilinda.

2. Yanipasa kuwa naye, kwani nategemea;
Anaweza kufariji na maneno matamu.

3. Yanipasa kuwa naye maisha yangu yote;
Yakiwapo majaribu na mashaka yo yote.

4. Yanipasa kuwa naye katika njia zangu;
Macho yake yaongoza hatua zangu zote.

WhatsApp