151 – Huniongoza Mwokozi

( 537 – He Leadeth Me )

1. Huniongoza Mwokozi, ndipo nami hufurahi,
Niendapo pote napo, ataniongoza papo.

Kuongoza hunishika; kwa mkono wa hakika;
Nitaandamana naye Kristo aniongozae.

2. Pengine ni mashakani nami pengine rahani;
Ni radhi, ijayo yote, yupo nami siku zote.

3. Mkono akinishika kamwe sitanung’unika;
Atakachoniletea ni tayari kupokea.

4. Nikiisha kazi chini sita kimbia mauti;
Kushinda ni ya hakika nikiongozwa na Baba.

WhatsApp