146 – Twae Wangu Uzima

( 330 – Take My Life and Let It Be )

1. Twae wangu uzima sadaka ya daima;
Twae saa na usiku Zikutukuze huku.

2. Twae mikono nayo, ifanye upendayo,
Twae yangu miguu, Kwa wongozi wako tu.

3. Twae sauti yangu, niimbe kwa Mungu tu;
Itwae na midomo, Ijae neno lako.

4. Twae dhahabu pia Na yote ya dunia;
Twae yangu hekima, upendavyo tumia.

5. Nia itwae, Mungu, haitakuwa yangu;
Twae moyo; ni wako, uwe makazi yako.

6. Twae mapenzi yangu, sifa za moyo wangu;
Twae kabisa nafsi Niwe wako halisi.

WhatsApp