137 – Saa Heri Ya Sala

( 501 – Tis the Blessed Hour of Prayer )

1. Saa heri ya sala tunapojidhili,
Kama tukija kwake yesu rafiki.
Tukiwa na imani kwamba yu mlinzi,
Waliochoka sana watapata raha.

Saa ya sala, iliyo heri;
Waliochoka sana watapata raha.

2. Saa heri ya sala, ajapo mwokozi,
Ili awasikie watoto wake.
Hutwambia tuweke miguuni pake
Mizigo yetu yote: tutapata raha.

3. Saa heri ya sala, wawezapo kuja
Kwa Bwana Yesu wanaojaribiwa;
Moyo wake mpole, atawarehemu;
Waliochoka sana watapata raha.

4. Saa heri ya sala tutakapopewa
Mibaraka ya roho, tukimwamini;
Kwa kuamini kweli hatutaogopa;
Waliochoka sana watapata raha.

WhatsApp