132 – Bwana Ni Mchunga

( 546 – The Lord's My Shepherd )

1. Bwana ni Mchunga, Sitahiji;
Majani mabichi mlisho yangu.
Ananinywesha maji Matulivu;
Atanirudisha nikipotea.

2. Nipitapo bondeni mwa mauti
U mlinzi wangu—sitaogopa;
Fimbo lako latoshakunilinda;
Ukinifariji sina hasara.

3. Kati ya mateso mea waandaa,
Na kikombe changu kinafurika;
Umenipaka kichwani mafuta;
Nitaulizaje zaidi kwako?

4. Wema na fadhili zinifuate
Siku zangu zote hata milele;
Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana
Katika ufalme wa pendo lake.

WhatsApp