127 – Nisalama Rohoni Mwangu

( 530 – It Is Well With My Soul )

1. Nionapo amni kama shwari, au nionapo shida;
Kwa hali zote umenijulisha ni salama rohoni mwangu.

Salama rohoni,
Ni salama rohoni mwangu.

2. Ingawa Shetani atanitesa, nitajipa moyo kwani,
Kristo ameona unyonge mwangu; amekufa kwa roho yangu.

3. Dhambi zangu zote, wala si nusu, huwekwa msalabani;
Wala sichukui laana yake, ni salama rohoni mwangu.

4. Ee Bwana himiza siku ya kuja, panda itakapolia:
Utakaposhuka sitaogopa ni salama rohoni mwangu.

 

WhatsApp