118 – Nilipotoka Kabisa

( 296 – Lord, I'm Coming Home )

1.Nilipotoka kabisa, sasa narudi
Nikakawia dhambini, Bwana narudi.

Narudi nyumbani: daima kwako.
Kwa upendo nipokee: Naja nyumbani.

2.Nikasusurika sana, sasa narudi
Mwenye uchungu natubu, Bwana narudi.

3.Nimechoka maovuni, sasa narudi;
Pendo lako lanivuta, Bwana narudi.

4. Ndilo tumaini langu, sasa narudi;
Yesu alinifilia, Bwana narudi.

5. Damu yake yanitosha, sasa narudi;
Unioshe kenyekenye, bwana narudi.

WhatsApp