115 – Naendea Msalaba

( 307 – I Am Coming to the Cross )

1. Naendea msalaba, Ni mnyonge, mpofu,
Yapitayo naacha nipe msalaba tu.

Nakutumaini tu, wee Mwana wa Mungu;
Nainamia kwako; Niponye sasa, Bwana.

1. Nakulilia sana: Nalemewa na dhambi;
Pole Yesu asema: “Nitazifuta zote.”

3. Natoa vyote kwako, nafasi nazo nguvu,
Roho yangu na mwili viwe vyako milele.

4. Kwa damu yake sasa amenivuta sana,
Upendo hubidisha, nimtafute Mwokozi.

WhatsApp