113 – Bubujiko

( 336 – There Is a Fountain )

1. Damu imebubujika, Ni ya Imanweli,
Wakioga wenye taka, Husafiwa kweli.

2. Ilimpa kushukuru Mwivi mautini;
Nami nisiye udhuru, Yanisafi ndani.

3. Kondo-o wa kuuawa, Damu ina nguvu,
Wako wote kuokoa kwa utimilivu.

4. Bwana, tangu damu yako Kunisafi kale,
Nimeimba sifa zako. ‘taimba milele.

5. Bwana, umenikirimu Nisiyestahili
Kwa damu yako, sehemu Ya mali ya kweli.

6. Nikubali kumwimbia Mbinguni milele.
Mungu nitamsifia Jina lako pweke.

WhatsApp