107 – Nipo Bwana, Nitume

( 359 – Hark! the Voice of Jesus Calling )

1. Sauti ni yake Bwana, “Kwenda, nani tayari”
Mavuno yanakawia, Nani atayavuna?
Kwa kudumu amaita, Zawadi atatoa;
Nani atakayejibu “Nipo Bwana, nitume.”

2. Kana huwezi safari Hata Nchi za mbali,
Pana watu karibuni Wasio mjua Yesu;
Kama huwezi kusema Jinsi ya malaika,
Waweza kuutangaza Upendo wa mwokozi.

3. Ingawa huwezi kuwa Mkesha mlangoni,
Ukiwatolea watu Nafasi ya uzima;
Kwa sala na kwa sadaka Watoa msaada,
Kama Harun mwaminifu, Kuinua Mikono.

4. Roho za watu zikifa, Bwana akikuita,
Usiseme kwa uvivu, “Hakuna kazi kwangu.”
Kwa furaha anza kazi Ile akiyokupa,
Ukajibu mara moja “nipo Bwana, nitume.”

WhatsApp