106 – Huna Kitu Kwa Yesu?

( Nothing for Jesus )

1. Ukitafuta mali, Huna wasaa kwa Yesu?
Kwa matendo ya haki Huna wasaa kwa Yesu?
Ansa za kunia, Mambo yako ya raha
Haya unatafuta; Huna wasaa kwa yesu?

2. Mambo yanakusonga: Kwake huna nafasi?
Watekwa na dunia, Kwake huna nafasi?
Humwani m-langoni, Anapopiga hodi?
Daima hukusihi: Kwake huna nafasi?

3. Sa-a ni za thamani, Kwake huna nafasi?
Wala hamfnyi bidii, Kwake hamnayo kazi?
Hamkufika kwao Waliomo shimoni
Na waliopotea? Kwake hamnayo kazi?

4. Na wazaa majani tu? Huna tunda kwa Yesu?
Mikono i mitupu, Huna tunda kwa Yesu?
Huna chembe kwa ghala kazi yako kulipa;
Wala huna furaha Unapomwona Yesu?

WhatsApp