170 – Jina Langu Limeandikwa Je?

( Lord, I Care not for Riches )

1. Siitafuti mali, wala utajiri;
Nataka kwa yakini nipate Mwokozi.
Chuoni mwa Ufalme, niambie Yesu,
Jina langu yakini limeandikwa, Je?

Limeandikwa, Je? Jina langu huko?
Kitabuni mbinguni, limeandikwa je?

2. Dhambi zangu ni nyingi, ni kama mchanga,
Lakini damu yako, Mwokozi, Yatosha;
Kwani umeahidi: zijapo nyekundu
Zitakuwa nyeupe ilivyo theluji.

3. Mji mzuri sana, wa majumba makuu,
Walipo malaika, mji bila ovu;
Wakakapo walio na mavazi safi,
Limeandikwa sasa, jina langu huko?

WhatsApp