140 – Hivi Nilivyo Unitwae

( 314 – Just as I Am )

1. Nitwae hivi nilivyo, umemwaga damu yako,
Nawe ulinyoniita, Bwana Yesu, sasa naja.

2. Hivi nilinyo; si langu kujiosha roho yangu;
Nisamehe dhambi zangu, Bwana Yesu, sasa naja.

3. Hivi nilivyo; sioni kamwe furaha moyoni,
Daima ni mashakani, Bwana Yesu, sasa naja.

4. Hivi nilivyo kipofu, maskini na mpungufu;
Wewe ndiwe u tajiri, Bwana Yesu, sasa naja.

5. Hivi nilivyo, mimi tu, siwezi kujiokoa;
Na wewe hutanikataa, Bwana Yesu, sasa naja.

6. Hivi nilivyo; mapenzi yamenipa njia wazi;
Hali na mali sisazi, Bwana Yesu, sasa naja.

WhatsApp